Sunday, May 13, 2012

YANGA HALI BADO SI SHWARI.. VIJANA HAWAMTAKI NCHUNGA


Umoja wa vijana wa klabu ya soka ya Yanga ya jijini Dar es Salaam leo wamekutana katika makao makuu ya klabu hiyo ili kujadili mstakabali wa timu yao pamoja na usajili wa msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania bara.

Mkutano huo pia umejadili hatma ya mwenyekiti wa klabu hiyo Lloyd Nchunga, usajili wa msimu ujao pamoja na mambo yaliyojitokeza kwenye mkutano ulioitishwa katikati ya wiki na Nchunga klabuni hapo.

Mwenyekiti wa vijana wa klabu hiyo Bakili Magele amesema yeye pamoja na vijana wenzie wataendelea na  msimamo wao wa kumtaka Nchunga ajiuzuru Pamoja na kamati ya utendaji ya klabu hiyo.

Baadhi ya vijana na wafurukwa wa Yanga wakapaza sauti zao na kuutaka uongozi wa klabu hiyo kuachia ngazi ikiwa ni pamoja na kamati ya utendaji ya Yanga.

Katika maoni yao wanchama wamelalamikia uongozi uliopo madarakani kwa kushindwa kuitisha mikutano mkuu jambo ambalo ni kinyume na katiba ya Yanga.


Mwisho.


No comments:

Post a Comment