Sunday, May 13, 2012

TBL KUHAMASISHA MICHEZO VYUONI



Kampuni ya bia Tanzania TBL kupitia kinywaji chake cha Grand Malt wamefanya tamasha la michezo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu linalojulikana kama Excel Grand Malt lenye lengo la kuhamasisha michezo baada ya masomo.

Tamasha hilo limejumuisha michezo mablimbali ikiwemo mpira wa miguu, kikapu, kuvuta kamab pamoja na pool table na kushuhudia mshindi akijinyakulia kitita cha 
shilingi laki 5.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa tamasha hilo meneja masoko wa TBL Fimbo Butala amesema kuwa kwa kupitia kinywaji hicho watazunguka mikoa yenye vyuo vya elimu ya juu ili kuhamasisha michezo vyuoni.

Nao baadhi ya wanafunzi walioshirikikatika michezo mbalimbali wamesema kuwa ingawa kulikuwa na mvua lakini ushindani umeonekana baina ya washiriki hao.

Bonanza hilo litakuwa likifanyika kila mkoa kwa kuwashirikisha wanafunzi wa vyuo vikuu vya mikoa husika ili kuhamasisha michezo baada ya muda wa masomo kwa wanafunzi hao.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment