Sunday, May 13, 2012


MASHINDANO YA NETBALI AFRIKA YAMALIZIKA MALAWI MABINGWA TENA

Timu ya Taifa ya mpira wa pete Taifa Queens imefanikiwa kupata tiketi ya kucheza michuano ya viwango vya dunia baada ya kuichapa timu ya Taifa ya Botswana na kushika nafasi ya pili katika fainali za Afrika zilizomalizika jana jijini DSM.

Malkia hao wa Tanzania wameshika nafasi hiyo baada ya kuishushia kipigo cha mabao 32 kwa 23 Botswana katika mchezo mkali uliochezwa kwenye uwanja wa ndani wa Taifa.

Mchezo huo uliokuwa wa mwisho katika michuano hiyo ulilazimika kuahirishwa kutoka saa NANE mchana hadi saa MOJA usiku baada ya kushindwa kuchezwa katika viwanja vya nje kutokana na mvua kubwa uliyonyesha mfululizo jijini DSM.
 
Katika hali ya kustaajabisha…uwanja wa ndani nako mambo hayakuwa shwari kabisaaa…pale ambapo mvua iliamua kuwafuata wachezaji na kuharibu ladha yote ya mchezo,ikiwa ni pamoja na juhudi za makusudi za mwamuzi wa mchezo huo na baadhi ya viongozi kushiriki zoezi la kupiga deki uwanja….

Hii inakuwa mara ya kwanza kwa Taifa Quens kukamata nafasi hiyo na sasa imepanda viwango kutoka vya  Afrika hadi Dunia.

Mgeni rasmi katika mchezo huo Mke wa Makamu wa Rais Aisha Bilal aliyeambatana na mke wa Waziri Mkuu Tunu Pinda amewakabidhi wachezaji wa Taifa Queens kombe la ushindi wa pili na mabingwa wapya wa michuano hiyo Malawi ambao wametetea ubingwa wao,na Zambia ambao wameshika nafasi ya tatu.

Nchi ambazo zimeshiriki michuano hiyo ni Lesotho, Zambia, Malawi ,Botswana, Zimbabwe na mwenyeji Tanzania.


Mwisho.









No comments:

Post a Comment